UNATATIZO L NGUVU ZA KIUME,HAPA PANAKUHUSU
SABABU ZA UPUNGUFU AU UKOSEFU WA NGUVU ZA KIUME
1.Vyakula hasa vyenye mafuta ya wanyama au mafuta yenye Lehemu(Cholestrols).
Matumizi ya vyakula vye kusindikwa zaidi.
2.Madawa, dawa kama Cimetidine ya vidonda vya tumbo au Adolmet ya shinikizo la damu la kupanda.
3.Miozi kama ya X-ray, Gamma Ray, simu,na vifaa vingine vya Electronic .
4.Magonjwa kama Sonona, Msongo wa mawazo, Kisukari, Kifafa, Ngiri n.k
5.Unene kupita kiasi(Obesity).
6.Kupendelea kuangalia picha za ngono au utupu.
7.Sigara.
8.Pombe.
9.Na nyinginezo.
Hizo ni baadhi ya sababu kwa ujumla wake.
Vyakula vyenye madini ya zinc, folic acid,Omega 3(Mafuta ya samaki), Vitamini B1, B6,B12, E n.k ni katika vyakula vyenye kuongeza hamu ya tendo la ndoa. Pia kuongeza ufanisi wa ufanyaji wa tendo la ndoa(Nguvu).
Baadhi ya vyakula hivyo ni vifuatavyo:
Tangawizi, Kitunguu swaum, Tikiti maji(hasa mbegu zake), Parachichi,Kitunguu maji, Asali, Habat sawda, Tende,Pilipili, Mdalasini, Karanga, Korosho,Pweza, Kiini cha yai, Mkate wa brown,Dark Chocolate, Mbegu za boga, Soya,Karoti, Ndizi mbivu n.k.
Vyakula hivi unaweza kula katika namna ya kuimarisha na kuboresha afya yako,lakini unaweza ukala katika namna ya kuimarisha hamu ya tendo la ndoa(Libido). Kwa leo tutaelezea juisi ya tende na tikiti maji.
Kwa mfano Juisi ya Tende hii ina matokeo ya haraka kama tatizo lako siyo sugu.
JUISI YA TENDE
Chukua tende kiasi kama robo kilo zitoe kokwa ,weka kwenye blenda,tia maziwa fresh kidogo zisage,na utaongeza maziwa kadri uzito wa juisi utakaohitaji na usitie sukari.
Juisi hii unaweza ukaongeza na unga wa habat sawda, unga wa tangawizi na unga wa karanga au soya kiasi kama kijiko cha chai.
Na kama hauna blenda basi kunywa maziwa fresh na tende,na unaweza ukaongeza na karanga mbichi na kipande cha tangawizi au ukatia unga wa tangawizi katika maziwa ya moto pamoja na Habat sawda ya unga na ukaweka asali.
Pia katika juisi ya tende unaweza ukaweka na asali kidogo.
Na unaweza ukatengeneza mchanganyiko wa Asali,Habat sawda,Tangawizi ya unga,Mdalasini ya unga, Kitunguu sawm (Garlic paste) ukawa unatumia kama jam au ukala vijiko viwili asubuhi na jioni huku ukitafunia na karanga au korosho au Brown bread.
JUISI YA TIKITI MAJI.
Andaa juisi ya tikiti maji bila ya kutoa mbegu, weka jikoni kamulia Limao kidogo na ikianza tu kuchemka itoe jikoni,kunywa.
Hivi ni baadhi ya vyakula vinavyopatikana katika mazingira yetu.Tujitahidi kuvitumia ili kuoberesha afya zetu.


0 Comments:
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home